banner

April 26, 2024

MAN CITY YAICHAPA 4-0 BRIGHTON & HOVE ALBION

MAN CITY YAICHAPA 4-0 BRIGHTON & HOVE ALBION


MABINGWA watetezi, Manchester City wameibuka na ushindi mabao 4-0 dhidi ya wenyeji, Brighton & Hove Albion Uwanja wa The Amex, Falmer, East Sussex.
Mabao ya Manchester City yamefungwa na kiungo mkongwe Mbelgiji, Kevin De Bruyne dakika ya 17 na washambuliaji Muingereza, Philip Foden mawili dakika ya 26 na 34 na' Muargentina, Julián Álvarez dakika ya 62.
Kwa ushindi huo, Manchester City wanafikisha pointi 76 katika mchezo wa 33 ikizidiwa pointi moja na vinara, Arsenal ambao pia wamecheza mechi moja zaidi, wakati Brighton & Hove Albion inafikisha pointi 44 katika mchezo wa 33 nafasi ya 11.



source http://www.binzubeiry.co.tz/2024/04/man-city-yaichapa-4-0-brighton-hove.html

Post a Comment

Whatsapp Button works on Mobile Device only

Start typing and press Enter to search